YAJUE MAMBO HAYA MA 5 ILI USIWAKELE WENGINE KATIKA MATUMIZI YA SIMU
Na Godfrey Mgaya
Ni kitu cha kwanza wengi wetu tunakitazama asubuhi na kitu cha mwisho kukiangalia usiku.Simu zetu haziko mbali nasi na tunaziangalia kila baada ya dakika 12, kwa mujibu wa mamlaka ya kudhibiti mawasiliano nchini Uingereza, Ofcom.
Ni mahusiano ambayo yanaonekana kuwa yatadumu zaidi, hivyo tunakudokeza sheria tano za matumizi ya simu ambayo yanapaswa kutazamwa kwa umakini.
1.Kuzungumza na simu wakati wa kula chakula
Watu wengi hufanya hivyo, na zaidi ya 26% ya vijana wanakubali suala hili
''Simu zinapaswa kuwa zimezimwa saa zote wakati wa chakula, mikutano na sherehe,''anasisitiza Diana Mather, mshauri wa masuala ya tabia.
''Mtu uliyenaye ni mtu aliye muhimu zaidi.Hakuna miongoni mwetu asiye na umuhimu.
Chimbuko la Illuminati na dhana kuhusu nguvu zao
Hata kutazama televisheni inakuwa imezimwa kwa baadhi ya watu wakati mkiwa kwenye meza ya chakula
Zaidi ya watu wanne kati ya watano walio na umri wa miaka 55 na zaidi wanafikiri haikubaliki kutazama ujumbe wa simu ukilinganisha na 46% ya umri wa miaka 18 mpaka 34.
2. Kusikiliza muziki wenye sauti kubwa kwenye usafiri wa Umma
Kitaalamu huitwa sodcasting yaani tabia ya kusikiliza muziki kutoka kwenye simu au vifaa vingine kwa sauti kubwa bila kujali wanaokuzunguka.
Inahusisha kutazama video au kucheza michezo ya kwenye simu kwa sauti kubwa.
76% kati yetu tunalipinga lakini hatuachi tabia hiyo.
3.Kuzungumza na simu wakati unapotakiwa kumsikiliza mtu mwingine
''Kutuma ujumbe na kuzungumza ni tabia mbaya sana,''anasema mtaalamu Diana Mather.
Ikiwa hatupeani muda sisi wenyewe, tunapoteza nafasi kubwa sana ya kufahamiana vizuri''.
Wanasiasa wenzake John McDonnell huenda walikosa kumfahamu kansela kivuli wakati wa kipindi cha bunge la commons kikiendelea
Alikuwa na cha kusema wakati wa kutoa taarifa mwaka 2016 lakini wenzake walikuwa wakitazama simu zao za mkononi.
4. Kutembea huku ukitazama simu yako
Huinamisha vichwa, macho yakiwa kwenye kioo cha simu, wanakuja upande ambao upo.Kimoyomoyo unapiga kelele tazama mbele! tazama mbele!
Na mtumiaji wa Twitter @tiredhorizon ametoa onyo kwa Umma weka simu yako mbali unapokuwa kwenye majengo ya umma, hospitali na karibu na maeneo magari aina ya malori yanapogeuza
Alisema amekuwa akishuhudia watu wakijigonga kwenye mbao za matangazo, au wakiwagonga wagonjwa wakiwa kwenye vitanda hospitalini.
5. Kutazama simu yako wakati ukiwa na wengine mkitazama televisheni
Kati ya watu 10, wanne (41%) ya watu wazima wanaona kuwa haikubaliki kutumia simu wakati uko na familia kwenye sofa mkitazama televisheni.
Hakuna maoni